Habari Ya Ndani
Mashuhuda wa bomu lililotupwa kanisani ;walishuhudia lilivyotua chini mpaka linalipuka
Kwa ufupi
- Kwa wakati huo, hata maumivu nilikuwa siyasikii, nikataka kukimbia, ardhi siioni, ninaona tu kama napelekwa huku na huku, nikasema nitashindana na hizi nguvu mpaka saa ngapi, nikasema ngoja nitulie.
Mei 5 mwaka 2013 ni siku ambayo haitafutika
katika historia ya Tanzania kutokana na tukio la kusikitisha la kutupwa
kwa bomu kanisani, ambapo watu watatu walifariki na wengine zaidi ya 60
kujeruhiwa.
Tukio hilo lilitokea mbele ya Balozi wa Vatican na
Mwakilishi wa Papa nchini Tanzania, Askofu Mkuu Francisco Montecillo,
Askofu Mkuu Josephat Lebulu wa Jimbo Kuu la Arusha, walipokuwa
wakizindua jengo la Kanisa Katoliki, Parokia ya Mtakatifu Joseph
Mfanyakazi, Olasiti, Arusha.
Siku hiyo iliyoleta historia mbaya kwa taifa letu
kutokana na tukio hilo ambalo viongozi mbalimbali waliliita la kigaidi,
halitaweza kusahaulika kwa baadhi ya watu ambao wanasimulia:
Fatma Tarimo (39), mkazi Olasiti mkoani Arusha.
Yeye, ambaye ni mama wa watoto watano, anasema siku ya tukio aliamka
asubuhi akiwa ni mtu mwenye furaha kuliko siku zote huku akiwa shauku ya
kumaliza shughuli zake mapema kisha awahi kanisani.
Anasema kuwa kabla ya kujiandaa kwenda kanisani aliwatayarisha watoto wake ili watangulie.
Mama huyo ambaye ni Mwalimu wa Shule ya Msingi
Burka Estate, anasema baada ya watoto wake kuondoka yeye alibaki
nyumbani ili kumtayarishia chakula mama yake aliyekuwa amemtembelea.
Anaeleza kuwa, baada ya kumaliza shughuli zake
alijiandaa na kwenda kanisani ambapo alipata lifti ya gari la watawa wa
kanisa hilo.
“Pale kuna misa mbili, siku nyingine watoto huwa
wanakwenda misa ya pili, lakini siku ile kwa sababu ya ufunguzi wa jengo
la kanisa kulikuwa na misa moja, mimi nikasema watoto watangulie
kanisani na mimi nimtayarishie kwanza mama chakula,” anasema.
Anasema kuwa, walipofika kanisani walikaa nyuma
huku mbele kukiwa na viongozi mbalimbali wa kanisa hilo, watawa, pamoja
na vikundi mbalimbali vya kwaya.
Aeleza bomu lilivyolipuka
Bomu lile halikutua mbali sana na nilipokuwa,
ilikuwa kama umbali wa hatua moja tu na lilipotua chini watu walisogea
pembeni kidogo na eneo lile kulikuwa na watoto wengi.
Nakumbuka wakati huo misa ilikuwa inaendelea na
viongozi walikuwa wamesimama tayari kwa kuzindua jengo, niliona kitu
kama chuma kimerushwa kikatua pembeni mwangu.
- Vurugu hizi za Mtwara zitoshe kuwa fundisho, somo kwetu
- Faini juu, ajali bado zinaongezeka
- Kutana na mashuhuda wa bomu lililoua Arusha
- Hukumu kesi ya uporaji wa Sh239 mil za NMB sasa kutolewa Juni 4
- ‘Acheni maandamano ya kijinga’
- Kesi ya Richmond kufufuliwa
- ‘Mgogoro wa Fahari wawili’ waendelea
- Watu wengine 10 wakamatwa Iringa
- Usajili: Wafahamu wachezaji waliopo sokoni
- Umuhimu wa viwanja vya michezo unasahaulika
- Waliofeli kidato cha nne waula, ufaulu sasa waongezeka
- Sitta ataja wanaotetea nchi
- Jeshi lafanikiwa kudhibiti vurugu Mtwara
- Lema amvaa Lowassa kwa helikopta Monduli
- Upo uwezekano wa kupata rais mwanamke, 2015?
- Wawekezaji 45 kuwekeza Mtwara
- JWTZ wakanusha taarifa za askari kujihusisha na makahaba DRC
- Wizara ya Elimu yapangua ratiba rasmi ya Bunge
- Usajili: Wafahamu wachezaji waliopo sokoni
- Kagera: Simba wametuliza
No comments:
Post a Comment