Wednesday 7 August 2013

NYUKI NA VIJANA WA KITANZANIA TWAWEZA ONDOA TATIZO LA AJIRA TANZANIA

Mzinga wa nyuki ni mahali au nafasi ambako kundi la nyuki inakaa pamoja na nsega. Porini nyuki wanatafuta tu shimo lolote au pango na kujenga nsega ndani yake. Baada ya kujua faida za asali watu wameanza kutengeneza mizinga ya nyuki yaani nafasi zinazofaa ili kuvuta nyuki waingie. Namna ya mzinga wa kidesturi katika Afrika ni nusu mbili za kipande cha mgogo kombe zinazofungwa kwa kamba na kuacha nafasi katikati. Nyuki wanaotafuta nafasi wanapenda kuingia na kuanzisha kundi jipya mle. Tatizo ni mavuno ya asali maana yake ni lazima kufungua mzinga wote na tokeo lake pamoja na mavuno mara nyingi ni kuharibu kundi la nyuki ndani ya mzinga hasa kwa sababu malkia anauawa. Mizinga ya kisasa inaepukana na tatizo hili kwa muundo tofauti wa mzinga. Mzinga huwa sanduku lenye fremu kadhaa ndani yake. Nyuki hutumia fremu kujenga nsega ndani ya fremu. Wakati wowote fremu inaweza kutolewa katika mzinga na kuangaliwa, kutolewa asali na kurudishwa bila kuua nyuki.